ADA ZA UANACHA - 2007
Bofya
hapa kwa kuomba uanacha mwaka 2007
Uamuzi kuhusu viwango vya ada za uanachama za Umoja wa Kimataifa wa
Wadau wa Mbuzi ulifikiwa wakati wa mkutano wa Bodi uliofanyika mwezi
Juni 2006 nchini Romania. Ikiwa kama mkakati wa Umoja wa Wadau wa Mbuzi
Kimataifa wa Kuboresha utafiti na maendeleo ya mbuzi duniani kwa manufaa
ya binadamu bodi iliamua kupunguza ada ya uanachama kwa watu wanaoishi
katika nchi ambazo kiwango chao ni chini ya .500 kulingana na Vielelezo
vya umoja wa mataifa vya maendeleo ya Binadamu. Kufahamu
zaidi kuhusu Vielelezo vya umoja wa mataifa vya maendeleo ya Binadamu
bofya hapa
Maendeleo ya Binadamu ni zaidi ya kupanda au kushuka kwa pato la taifa.
Maendeleo ya binadamu yanahusiana na kujenge mazingira ambayo watu watatumia
ujuzi walionao kuongeza uzalishaji, kuishi maisha ya ubunifu kulingana
na mahitaji na matakwa yao. Watu ndio utajiri halisi wa mataifa. Kwa
hiyo maendeleo yanahusu kuwawezesha watu waweze kuwa na uchaguzi wa
kuishi maisha wanayo yathamini.~Umoja wa Mataifa
Kulingana na wazo hilo, uamuzi huo wa Bodi utawawezesha watafiti, wazalishaji
na maafisa ugani wanaoishi katika nchi hizo kuweza kupata taarifa sahihi
na kupanua mtandao wa umoja wa wadau wa mbuzi kimataifa
Vielelezo vya umoja wa mataifa vya maendeleo ya Binadamu (UN-HDI) ni
vielelezo mchanganyiko ambavyo vinapima mafanikio katika maeneo makubwa
matatu ya maendeleo ya binadamu
- Maisha marefu na yenye afya (ambayo hupimwa na matarajio ya muda
wa mtu wa kuishi)
- Elimu/maarifa (ambayo hupimwa kwa kuangalia uwezo wa kujua kusoma
na kuandika na kiwango cha uandikishwaji wa wanafunzi)
- Ubora wa maisha ( ambao hupimwa na pato la taifa na mlingano katika
uwezo wa kununua bidhaa mbalimbali)
Kuanzia Januari mosi 2007 viwango vya ada za uanachama kwenye Umoja
wa Kimataifa wa Wadau wa Mbuzi utagawanyika katika makundi
mawili yaani, kundi la juu na kundi la chini. Wale watakaoomba uanachama
wa Umoja wa Kimataifa wa Wadau wa Mbuzi ambao wanatoka
katika nchi ambazo zipo chini ya .500 kulingana na Vielezo vya umoja
wa mataifa vya maendeleo ya Binadamu watawekwa katika kundi la chini.
Watu watakaoomba uanacha Umoja wa Kimataifa wa Wadau wa Mbuzi
ambao wanatoka katika nchi ambazo zinaanzia .500 na kuendelea kulingana
na Vielezo vya umoja wa mataifa vya maendeleo ya Binadamu watawekwa
katika kundi la juu.
Ada za uanchama kwa kundi la chini zitapunguzwa na kufikia
- Dola za Kimarekani 20 kwa wanachama wa kawaida* ambao pia wanatumia
mtandao kupata taarifa za tafiti mbalimbali zinazohusu wanyama wadogo
wanaocheua
- Dola za Kimarekani 60 kwa wanachama ambao watajiandikisha kwa kujaza
fomu maalumu pia watapata taarifa za tafiti mbalimbali kupitia mtandao
zinazohusu wanyama wadogo wanaocheua
Ada za uanchama kwa kundi la juu zitapandishwa na kufikia
- Dola za Kimarekani 45 kwa wanachama wa kawaida* ambao pia wanatumia
mtandao kupata taarifa za tafiti mbalimbali zinazohusu wanyama wadogo
wanaocheua
- Dola za Kimarekani 145 kwa wanachama ambao watajiandikisha kwa kujaza
fomu maalumu* pia watapata taarifa za tafiti mbalimbali zinazohusu
wanyama wadogo wanaocheua
*Uanachama wa katika Umoja wa Kimataifa wa Wadau
wa Mbuzi ni pamoja na kupata taarifa mbalimbali kwa mtandao zinazohusu
wanyama wadogo wanaocheua kuanzia mwezi Januari na kumalizika mwezi
Desemba.
Kwa
orodha ya nchi mbalimbali kufuata alfabeti kulingana na viwango vya
umoja wa mataifa vya maendeleo ya Binadamu bofya hapa
Kwa
orodha ya nchi mbalimbali kulingana na viwango vya umoja wa mataifa
vya maendeleo ya Binadamu bofya hapa
Ili kuweza kufidia sehemu ya punguzo hili la ada ya uanachama, kiwango
cha ada ya uanachama kwa kundi la juu kimeongezwa kwa dola za kimarekani
tano ($5) kutoka katika kiwango chake cha sasa. Hata hivyo ongezeko
hili kidogo haliwezi kutosheleza kiwango cha fedha ambacho umoja wa
wadau wa mbuzi kimataifa unatarajia kupunguza kwa wanchama wake wa kundi
la chini. Kama unafahamu taasisi au shirika lolote ambalo lipo tayari
kutusaidia kutoa ruzuku kwa sehemu au kwa ada yote ya uanachama tafadhali
tujulishe.
Kwa taarifa zaidi kuhusu Vielelezo vya umoja wa mataifa vya maendeleo
ya Binadamu tembelea http://hdr.undp.org/hd/
Au http://en.wikipedia.org/wiki/Human_Development_Index
Bofya
hapa kwa kuomba uanacha mwaka 2007
Ukihitaji maelezo zaidi wasiliana na: goats@heifer.org